Monday, 24 August 2015

WANAUME KUKOSA WAKE




Visa vya wanaume kulalama kukosa jiko katika kisasi cha sasa vinaongezeka kurokana picha wanawake wanaleta katika maisha ya kila kuchao.
Nazungumza haya nikikumbuka kisa cha ntanashati mmoja aliyefungua roho na kutaja wazi kwamba imekuwa vyema kwake kuamua atakayekuwa mke wa kudumu naye kati ya mabinti wengi anaowapata. Anaeleza kuwa hofu yake inatokana na jinsi mabinti wengi huvalia nusu uchi, hawakingi miili yao vizuri kwa kukinga sehemu nyeti. Mtanashati huyo aitwae Robert anasema kwamba ni rahisi kupata kipusa wa kuwapeleka deti, kula hepi na kustarehe kitandani bali si wa kuoa na kuishi naye daima dawamu.
Inabainika wazi kuwa wanaume wengi wanaafadhalisha wanawake wenye taadhima na moyo mkunjufu wa kunyenyekea kando na wenye sura jamala au mavazi za ulimbwende. Hali kadhalika, wanaume hawapendi mabinti walevi wenye lugha chafu ya kukera. Kupata binti wa kuaminika na mwenye mienendo yanayompendeza mwanamume ni vigumu na hadimu kama maziwa ya kuku.

Wanaume wengu huchagua mbinu ya kuwabusa mabinti wengi kabla wengi kabla ya kupata anayefaa kama sulugu ya tatizo hili. Mbinu hii si dhabiti kwa kuwa inawalazimu kukosana na mabinti wengi kiasi cha kutotaka kuendelea na safari ya mapenzi. Inawapa wengi wazo la  kutompata anayempenda atawale roho kabla ya ndoa kwa kizinfizio kwamba sio yeye anayetawala moyo wake. Wengi wana taya spea zinazotoa ushindani mkali kwa hizo zilizo kazini, basi hazina budi kuebdelea.

Matikeo ya mbinu hii ni kwamba vipusa wengi wanabaki kutumiwa kama chombo cha majaribio kabla ya kutemwa ikiwa hawataafikia majaribio ya wanaume hao. Hili linasababisha kuvunjuka moyo kwa mabinti wengi na kusabambaratisha uhusiano wao na wanaume, hivyo basi kuwa chanzo cha kutoaminiana katika ndoa kutokana na wanaume kushindwa kudhibiti mchi baada ya kuchovyachovya bila tahadhari.

Wanahitaji wa kutendeana mema wala si wa kutendeana mabaya wa kupendana wala si kupendezana. Wa kukuza adabu pasipo kuadhibiana. Wa heri sio shari.

Hata hivyo wanaume pia wana kasoro katika mienendo yao haswa katika zile patashika za kutafuta mchumba ambavyo wanakisa uaminifu. Mara kwa mara hawajielezi kwa kina na kutangaza msimamo wao. Wanajipa sifa zisizo wafaa na kujitia hamnazo. Wanakiri bayana kuwa hawajawahi kosea binti yeyote maishani ilhali wao ndio wenye makosa.

No comments:

Post a Comment